Adventure
![]() |
RAFIKI,
UMETAMBUA MAISHA MAZURI YENYE KUONGOZWA NA ROHO MUTAKATIFU |
UNAWEZA KUSHINDA KILA SIKU KWA UWEZO WA ROHO MUTAKATIFU Mbele ya kupokea Kristo kuwa Mwokozi wako, wewe mwenyewe uliongoza maisha yako. (Isaya 53:6) Wakati ulipopokea Yesu Kristo, Roho Mutakatifu aliingia na kukaa ndani yako. (Waroma 8:9) Roho Mutakatifu anawezesha kila Mukristo kuwa na maisha ya furaha na ushindi. (2 Wakorinto 3:18) Sasa tuone namna BIBLIA INATUFUNDISHA JUU YA ROHO MUTAKATI FU Biblia inasema: 1 MUTU ASIYE NA KRISTOMutu asiye na Kristo ni yule hayapokea Kristo kuwa Mwokozi wake. Roho Mutakatifu hakai ndani yake. Biblia inasema: "Mutu wa tabia ya asili hapokei maneno ya Roho ya
Mungu: kwa sababu maneno haya ni upumbafu kwake; wala hawezi kuyafahamu, kwa
sababu yanatambulikana na roho." Tazama wa kwanza ... Picha hii
inaonyesha,
Maana ya picha hii.
|
Huyu
Mukristo . . . - Ameweka Kristo kuwa Mutawala kwa kiti. - Ana uwezo toka kwa Roho Mutakatifu - Analeta wengine kwa Kristo - Anaomba hata kupata majibu - Anafahamu Neno ia Mungu - Antii Mungu |
|
![]() |
Katika
maisha yake kunetokea - Mapendo - Furaha - Salama - Uvumilivu - Upole - Uaminifu - Wema |
Hivi tunaona ya kwamba
1 .Yesu yuko malshani kama Mwokozi wake.
2. Yesu yuko kwa kiti cha ukubwa, akimuongoza.
3. Sasa yeye ni mutumishi wa Yesu Kristo, na anamutii.
4. Kwa kadiri Mukristo anavyotii Roho Mutakatifu kumuongoza, matunda ya Roho
yanazidi kuonekana katika maisha yake, na anakuwa Mukristo imara.
Lakini Mukristo asiyeongozwa na Roho Mutakatifu ni sawa na
mutu wa namuna ya tatu...
3 MUKRISTO MWENYE TABIA YA MWILI
Mukristo mwenye kujiongoza anafikili zaidi juu ya kujipendeza kuliko kupendeza Mungu, sawa watu wa dunia wanafanya. Anafanana na mutoto muchanga anayetaka mambo yake tu.
Biblia inasema hivi juu ya Mukristo anayejipendeza.
"Na mimi, ndugu, sikuweza kusema na ninyi kama na
watu wa Roho, lakini kama na watu wa mwili; kama na watoto wadogo katika
kristo. Nimewakunywesha ninyi maziwa wala si chakula; kwa sababu mulikuwa
hamujakiweza, hata sasa hamukiwezi; kwa sababu hata sasa ninyi ni watu na
mwili; kwa sababu kuna wivu na ugomvi katikati yenu, ninyi si watu wa mwili
mukikwenda kwa namna ya watu.
1 Wakorinto 3:1-3
Sasa tazama ....
Picha hii mufano wa Mukristo wa
tabia ya mwili.
MUKRISTO MWENYE TABIA YA MWILI
Mukristo
huyu . . . - Hategemei Mungu kwa maneno yote - Hasaidii wengine kupatana na Kristo - Maombi si ya maana kwake - Hapendi sana kusoma Biblia - Mara nyingi mawezo yake ni mabaya |
|
![]() |
Mara nyingi . .
. - Anakuwa na wivu - Damiri yake inamutesa - Anaagaika na kuwayawaya - Anahukumu wengine - Anakata tamaa - Anakasirika - Anashindwa na tamaa zake |
Ujue kwamba:
1. Yesu angali katika maisha yake kama Mwokozi.
2. Lakin i mutu mwenvewe anaketi kwa kiti cha maisha yake na
kujitawala.
3. Yesu hana utawala wa kweli ndani ya maisha yake.
Mukristo mwenye tabia ya mwili, mara nyingine anataka kupendeza Mungu, lakini...
mara na mara anashindwa kufanya yaliyo mema.
"Maana sijui ninalofanya, kwa sababu lile ninalopenda
kufanya, silifanyi; lakini like nialochukia, ninalifanya. Kwa maana ninajua
kwamba ndanii yangu, maana ndani ya mwili wangu, halikai neno jema;
kwa sababu
kutaka ni kwangu, lakini kufanya lililo jema siwezi. Ole kwangu mimi mutu wa
taabu! Nani atakayeniokoa na mwili huu wa kufa?"
Waroma 7:15,18,24
Kwa hivyo
1. Mukristo we tabia ya mwili hana maisha ya furaha.
2. Mara na mara anaishi maisha ya kushindwa.
3. Wakati mwingine hatendi kama Mukristo hata kidogo.
Tufikili tena juu ye watu wale watatu.
NAMNA TATU YA WATU | ||
1. Mutu asiye na Kristo | 2. Mutu aliyejazwa na kuongozwa na Roho Mujtakatifu | 3. Mukristo wa tabi ya mwili |
![]() |
![]() |
![]() |
Picha gani inaonyesha maisha yako sasa?
Ungependa kuwa mutu wa namna gani kwa wale watatu?
NAMNA GANI MUKRISTO WA TABIA YA MWILI ANAWEZA KUPATA
MAISHA YENYE KUJAZWA (KUTAWALIWA) NA ROHO MUTAKATIFU?
TUNAJAZWA NA KUONGOZWA NA ROHO MUTAKATIFU KWA IMANI
Tunapata kuwa Wakristo kwa kuamini Yesu Kristo kuwa Mwokozi wetu. Vile tunajazwa na Roho Mutakatifu kwa imani, tukitegemea Mungu na kutii Neno lake.
Unaweza kumupa Roho Mutakatifu nafasi kukujaza na kukuongoza
sasa.
Kuna hatua tatu za kufanya.
1. UAMBIE MUNGU kwamba unataka maisha yanayojaa na kuongozwa na Roho Mutakatifu. "Heri wenye niaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa." Mathayo 5.6
2. UNGAMA ZAMBI ZAKO. "Tukikiri zambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee zambi zetu, na kutusafisha na uzalimu wote." 1 Yoane 1:9
Maana ya kuuongama ni nini?
a. Unakubali mbele ya Mungu kwamba umefanya zambi na kumukosea.
b. Unashukuru Mungu kwa kukusamehe na kukusafisha kwa damu ya Yesu
Kristo.
c. Unageuka toka zambi na kukubali kutii Mungu (Maana yake kutubu).
3 UJITOE KWA MUNGU
'Wala musitoe viungu vyenu kuwa vyombo vya kutumiwa kwa
zambi. Lakini mujitoe wenyewe kwa, Mungu kama wenye uhai nyuma ya kufa, na,
viungu vyenu kwa Mungu kuwa yvombo vya kutumiwa kwa haki."
Waroma 6:13
Kwa kuishi maisha ya kujazwa na kuongozwa na Roho
Mutakatifu, sharti kukubali Yesu atutawale katika mambo yote.
Inafaa atawale kila jambo katika maisha yetu, mali yetu, nyakati zetu, kazi zetu, ushirika na jamaa yetu, na ushirika na marafiki yetu.
Umefuata hatua hizi tatu? Uzisome tena
SASA UAMINI KWAMBA MUNGU ATAKUJAZA NA ROHO MUTAKATIFU NA KUKUONGOZA
Mungu atakujaza na Roho Mutakatifu na kukuongoza kama ukimuuliza kufanya hivi.
Kuna maneno mawili ya kukumbuka.
1. SHARTI TUTII AGIZO LAKE LA KUJAZWA NA ROHO MUTAKATI
FU
"Musilewe kwa mvinyo, ndani yake ni maketele, lakini mujazwe
Roho". Waefeso 5.18
2. SHARTI TUTEGEMEE AHADI YAKE YA KUTUJAZA NA ROHO
MUTAKATIFU
"Na huu ndio uhodari tulio nao mbele yake, ya kama tukiomba kitu
sawasawa na mapenzi yake, anatusikia. Na kama tukijua kwamba anatusikia, yo
yote tutakayomwomba, tunajua kwamba tumek wisha kupewa maombi
tuliyomuomba."
1 Yoane 5:14-15
HIVI
TUNAJAZWA NA ROHO MUTAKATIFU KWA IMANI
Njia moja ya kuonyesha imani yako, ni njia ya kuomba. KUOMBA KWAKO KUWE HIVI "Bwana Yesu, ninakuhitaji, uongoze maisha yangu. Nimejitawala mwenyewe katika maisha yangu. Sasa ninakubali mbele yako kwambe hii ni zambi. Ninaacha zambi hii na kujitoa kwako na kukutii, ili unitawale. Asante kwani umenisaimehe. Sasa ninatii agizo lako na kukuamini, unijaze na Roho Mutaketifu wako. Asante kunijaza kama ulivyoahidi." Unataka Mungu akujaze na kutawala maisha yako? NAMNA YA KUJUA KAMA
UMEJAZWA NA ROHO MUTAKATIFU
1.Moteur inaongoza camion. Hivi, UKWELI wa Munga unahitaji
kuongoza Mukristo NAMNA YA KUENDELEA KUONGOZWA ROHO MUTAKATIFU Ukifanya azmbi tena kwa kuongoza maisha yako, unahitaji kufanya maneno mawili. 1) Ungama zambi zako kwa Mungu. Atakusamehe na husafisha roho yako
tena. Ufuate hatua hizi mbili kila mara Roho Mutakatifu anakuonyesha zambi katika maisha yako. Hivi utakuwa na maisha ya furaha na ushindi. UTEGEMEE ROHO MUTAKATIFU KUENDELEA KUKUONGOZA NA KUKUJAAZA. HIVI YESU KRISTO ATAKUWA BWANA NA MUTAWALA WA KITI CHA MAISHA YAKO WAKATI WOTE. UAMINI MUNGU NA AHADIZAKE KATIKA BIBLIA Mukristo anaishi maisha yanayojaa na Roho Mutakatifu kwa imani tu. Wakati Roho Mutakatifu anaongoza maisha yako, utakuwa hivi: Sasa jambo linalokuha ni hili: INAFAA KWENDA KANISANI Ni sharti kujiunge kwa watu wanaokubali Yesu Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wao. Uhuzurie kanisa, kwenye watu wanaoamini UKWELI wa Biblia na kutii Bwana Yesu. Waebrania 10:25. KAMA KITABU HIKI KIMEKUSAIDIA, UKILETE KWA MUTU MWENGINE A 0 UMUSOMEE LIFE BUTEMBO, B.P. 5, ZAIRE
Kimeanclikwa na Dr. Wm. Bright |