Adventure

RAFIKI, UMETAMBUA MAISHA
MAZURI YENYE KUONGOZWA NA ROHO MUTAKATIFU

UNAWEZA KUSHINDA KILA SIKU

KWA UWEZO WA ROHO MUTAKATIFU

Mbele ya kupokea Kristo kuwa Mwokozi wako, wewe mwenyewe uliongoza maisha yako. (Isaya 53:6) 

Wakati ulipopokea Yesu Kristo, Roho Mutakatifu aliingia na kukaa ndani yako. (Waroma 8:9) 

Roho Mutakatifu anawezesha kila Mukristo kuwa na maisha ya furaha na ushindi. (2 Wakorinto 3:18)    

Sasa tuone namna…

BIBLIA INATUFUNDISHA JUU YA ROHO MUTAKATI FU

Biblia inasema: 
1 . Roho Mutakatifu ni Mungu. Matendo 5:3-5
2. Roho Mutakatifu anakaa ndani ya kila mutu aliyepokea kristo kuwa Mwokozi wake. 
    1 Wakorinto 3:16
3. Roho Mutakatifu ni Mwalimu wetu. Yoane 14:26 
4. Roho Mutakatifu anatusaidia katika uzaifu wetu. Waroma 8:26. 
5. Roho Mutakatifu ana uwezo kuliko pepo ao roho nyingine zote 1 Yoane 4:1-4
6. Roho Mutakatifu anazaa matunda ya roho katika maisha yetu. Wagalatia 5:22-23
7. Roho Mutakatifu anatupa uwezo wa kushuhudia Kristo. Matendo 1:8
                         Biblia inatuonyeshe juu ya watu wa namns tatu.

1 MUTU ASIYE NA KRISTO

Mutu asiye na Kristo ni yule hayapokea Kristo kuwa Mwokozi wake. 

Roho Mutakatifu hakai ndani yake. 

Biblia inasema:

"Mutu wa tabia ya asili hapokei maneno ya Roho ya Mungu: kwa sababu maneno haya ni upumbafu kwake; wala hawezi kuyafahamu, kwa sababu yanatambulikana na roho." 
1 Wakorinto 2:14

Tazama wa kwanza ...

Picha hii inaonyesha, 
MUTU ASIYE NA KRISTO

Kiti cha ukubwa ao cha 
utawala katik maisha
Mutu mwenyewe
Yesu Kristo

Maana ya picha hii. 
1. Yesu yuko inje ya maisha yake. 
2. Mutu asiye Mukristo anakaa kwa kiti cha ukubwa, akitawala maisha yake mwenyewe. 
3. Huyu anahitaji kupokea Yesu kuwa Mwokozi wake
                                          Sasa tuone mutu wa namna ya pili.. .


2  MUKRISTO ANAYEJAZWA NA KUONGOZWA NA   ROHO MUTAKATIFU

Wakati tunapokea Yesu Kristo kuwa Mwokozi wetu, Roho Mutakatifu anaingia na kukaa ndani yetu. (Waroma 8:9). Tukijaa na Roho Mutakatifu, tunakubali Yesu kututawala na kutuongoza. Tunapata maisha mazuri ya ushindi; vile tunawezeshwa kushuhudia Kristo (Matendo 1:8).
Biblia inaeleza juu ya maisha vanayojaa na Roho Mutakatifu.

"Matunda ya Roho ni mapendo, furaha, salama, uvumilivu, neema, wema, uaminifu, upole, ujizuiza, hakuna sheria juu ya maneno ya namna hii. " Wagalatia 5:22-23 
"Lakini mutapokea nguvu wakati Roho Mutakatifu anapokuja juu yenu, nanyi mutakuwa washuhuda wangu." Matendo 1:8

Tunapokubali Yesu Kristo kutawala maisha yetu, tunapendeza Mungu.

Picha hii inaonyesha Mukristo anayelaa na Roho jautakatifu 
MUKRISTO ANAYEONGOZWA NA ROHO MUTAKATIFU

Huyu Mukristo . . .
- Ameweka Kristo kuwa Mutawala kwa kiti.
- Ana uwezo toka kwa Roho Mutakatifu
- Analeta wengine kwa Kristo
- Anaomba hata kupata majibu
- Anafahamu Neno ia Mungu
- Antii Mungu
Katika maisha yake kunetokea
- Mapendo
- Furaha
- Salama
- Uvumilivu
- Upole
- Uaminifu
- Wema

Hivi tunaona ya kwamba 
1 .Yesu yuko malshani kama Mwokozi wake. 
2. Yesu yuko kwa kiti cha ukubwa, akimuongoza. 
3. Sasa yeye ni mutumishi wa Yesu Kristo, na anamutii. 
4. Kwa kadiri Mukristo anavyotii Roho Mutakatifu kumuongoza, matunda ya Roho yanazidi kuonekana katika maisha yake, na anakuwa Mukristo imara.
Lakini Mukristo asiyeongozwa na Roho Mutakatifu ni sawa na…

mutu wa namuna ya tatu...

3 MUKRISTO MWENYE TABIA YA MWILI

Mukristo mwenye kujiongoza anafikili zaidi juu ya kujipendeza kuliko kupendeza Mungu, sawa watu wa dunia wanafanya. Anafanana na mutoto muchanga anayetaka mambo yake tu. 

Biblia inasema hivi juu ya Mukristo anayejipendeza.

"Na mimi, ndugu, sikuweza kusema na ninyi kama na watu wa Roho, lakini kama na watu wa mwili; kama na watoto wadogo katika kristo. Nimewakunywesha ninyi maziwa wala si chakula; kwa sababu mulikuwa hamujakiweza, hata sasa hamukiwezi; kwa sababu hata sasa ninyi ni watu na mwili; kwa sababu kuna wivu na ugomvi katikati yenu, ninyi si watu wa mwili mukikwenda kwa namna ya watu. 
1 Wakorinto 3:1-3

Sasa tazama ....

Picha hii mufano wa Mukristo wa tabia ya mwili. 
MUKRISTO MWENYE TABIA YA MWILI

Mukristo huyu . . . 
- Hategemei Mungu kwa maneno yote
- Hasaidii wengine kupatana na Kristo
- Maombi si ya maana kwake
- Hapendi sana kusoma Biblia
- Mara nyingi mawezo yake ni mabaya
Mara nyingi . . . 
- Anakuwa na wivu
- Damiri yake inamutesa
- Anaagaika na kuwayawaya
- Anahukumu wengine
- Anakata tamaa
- Anakasirika
- Anashindwa na tamaa zake

Ujue kwamba: 
1. Yesu angali katika maisha yake kama Mwokozi. 
2. Lakin i mutu mwenvewe anaketi kwa kiti cha maisha yake na kujitawala. 
3. Yesu hana utawala wa kweli ndani ya maisha yake.

Mukristo mwenye tabia ya mwili, mara nyingine anataka kupendeza Mungu, lakini...

mara na mara anashindwa kufanya yaliyo mema.

"Maana sijui ninalofanya, kwa sababu lile ninalopenda kufanya, silifanyi; lakini like nialochukia, ninalifanya. Kwa maana ninajua kwamba ndanii yangu, maana ndani ya mwili wangu, halikai neno jema;
kwa sababu kutaka ni kwangu, lakini kufanya lililo jema siwezi. Ole kwangu mimi mutu wa taabu! Nani atakayeniokoa na mwili huu wa kufa?" 
Waroma 7:15,18,24

Kwa hivyo… 
1. Mukristo we tabia ya mwili hana maisha ya furaha. 
2. Mara na mara anaishi maisha ya kushindwa. 
3. Wakati mwingine hatendi kama Mukristo hata kidogo.

Tufikili tena juu ye watu wale watatu.

 

NAMNA TATU YA WATU
1. Mutu asiye na Kristo 2. Mutu aliyejazwa na kuongozwa na Roho Mujtakatifu 3. Mukristo wa tabi ya mwili

Picha gani inaonyesha maisha yako sasa? 
Ungependa kuwa mutu wa namna gani kwa wale watatu?

NAMNA GANI MUKRISTO WA TABIA YA MWILI ANAWEZA KUPATA MAISHA YENYE KUJAZWA (KUTAWALIWA) NA ROHO MUTAKATIFU?

TUNAJAZWA NA KUONGOZWA NA ROHO MUTAKATIFU KWA IMANI

Tunapata kuwa Wakristo kwa kuamini Yesu Kristo kuwa Mwokozi wetu. Vile tunajazwa na Roho Mutakatifu kwa imani, tukitegemea Mungu na kutii Neno lake. 

Unaweza kumupa Roho Mutakatifu nafasi kukujaza na kukuongoza sasa. 
Kuna hatua tatu za kufanya. 

1. UAMBIE MUNGU kwamba unataka maisha yanayojaa na kuongozwa na Roho Mutakatifu. "Heri wenye niaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa." Mathayo 5.6 

2. UNGAMA ZAMBI ZAKO. "Tukikiri zambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee zambi zetu, na kutusafisha na uzalimu wote." 1 Yoane 1:9 

Maana ya kuuongama ni nini? 
a. Unakubali mbele ya Mungu kwamba umefanya zambi na kumukosea. 
b. Unashukuru Mungu kwa kukusamehe na kukusafisha kwa damu ya Yesu Kristo. 
c. Unageuka toka zambi na kukubali kutii Mungu (Maana yake kutubu).

3 UJITOE KWA MUNGU

'Wala musitoe viungu vyenu kuwa vyombo vya kutumiwa kwa zambi. Lakini mujitoe wenyewe kwa, Mungu kama wenye uhai nyuma ya kufa, na, viungu vyenu kwa Mungu kuwa yvombo vya kutumiwa kwa haki." 
Waroma 6:13

Kwa kuishi maisha ya kujazwa na kuongozwa na Roho 
Mutakatifu, sharti kukubali Yesu atutawale katika mambo yote. 

Inafaa atawale kila jambo katika maisha yetu, mali yetu, nyakati zetu, kazi zetu, ushirika na jamaa yetu, na ushirika na marafiki yetu.

Umefuata hatua hizi tatu? Uzisome tena

SASA UAMINI KWAMBA MUNGU ATAKUJAZA NA ROHO MUTAKATIFU NA KUKUONGOZA

Mungu atakujaza na Roho Mutakatifu na kukuongoza kama ukimuuliza kufanya hivi. 

Kuna maneno mawili ya kukumbuka.

1. SHARTI TUTII AGIZO LAKE LA KUJAZWA NA ROHO MUTAKATI FU 
"Musilewe kwa mvinyo, ndani yake ni maketele, lakini mujazwe Roho". Waefeso 5.18 

2. SHARTI TUTEGEMEE AHADI YAKE YA KUTUJAZA NA ROHO MUTAKATIFU 
"Na huu ndio uhodari tulio nao mbele yake, ya kama tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, anatusikia. Na kama tukijua kwamba anatusikia, yo yote tutakayomwomba, tunajua kwamba tumek wisha kupewa maombi tuliyomuomba." 

1 Yoane 5:14-15

 

HIVI TUNAJAZWA NA ROHO MUTAKATIFU KWA IMANI 

Njia moja ya kuonyesha imani yako, ni njia ya kuomba. 

KUOMBA KWAKO KUWE HIVI 

"Bwana Yesu, ninakuhitaji, uongoze maisha yangu. Nimejitawala mwenyewe katika maisha yangu. Sasa ninakubali mbele yako kwambe hii ni zambi. Ninaacha zambi hii na kujitoa kwako na kukutii, ili unitawale. Asante kwani umenisaimehe. Sasa ninatii agizo lako na kukuamini, unijaze na Roho Mutaketifu wako. Asante kunijaza kama ulivyoahidi." 

Unataka Mungu akujaze na kutawala maisha yako? 
Sasa ungependa kuomba maombi haya?


NAMNA YA KUJUA KAMA UMEJAZWA NA ROHO MUTAKATIFU 
Uliomba Mungu akujaze na Roho Mutakatifu? Unaweza kujua kwamba umejaazwa Roho, kwa kuamini ahadi za Mungu katika Biblia 
USITEGEMEE MAFIKILI YAKO KWA KUKUONGOZA 
Siku nyingine utafurahi kwa mafikili yako, siku nyingine utakuwa na huzuni ao shaka, si neno. Mukristo wa kweli anasimama na imani, akitegemea Mungu na ahadi zake katika Biblia. Hivi ujue hakika kama amekujaza na Roho Mutakatifu, na kama anakuongoza na kukuwezesha.


1.Moteur inaongoza camion. Hivi, UKWELI wa Munga unahitaji kuongoza Mukristo 
2. Essence inaacha moteur kutumika. Hivi, IMANI ni kufuata na kutegemea UKWELI wa Mungu. 
3. Remorque inakokotva nyuma. Hivi MAFIKILI yanakokotwa nyuma. hayawezi kutongoza. 
4. Sisi tunategemea Mungu na ukwefl wake, hapana mafikili yetu . 
5. Kwa kuwa Munqu ni mwaminifu, unaweza kumushukuru sasa kwa kukujaza na Roho Mutakatifu, hata kama huoni umbalimbali wo wote.


NAMNA YA KUENDELEA KUONGOZWA ROHO MUTAKATIFU 

Ukifanya azmbi tena kwa kuongoza maisha yako, unahitaji kufanya maneno mawili. 

1) Ungama zambi zako kwa Mungu. Atakusamehe na husafisha roho yako tena. 
    (1 Yoane 1:9) Ugeuke toka zambi ya kujiongoza. 
2) Ujazwe tena na Roho Mutakatifu, akuongoze na kukuleteya uwezo wake.Uulize  Mungu kukuongoza katika maisha yako. Utii agizo lake ya kujaazwa na Roho Mutakatifu. (Waefeso 5:18). Utegemea Mungu na ahadi yake ya kukujaaza na Roho Mutakatifu. (1 Yoane 5:14.15). 

Ufuate hatua hizi mbili kila mara Roho Mutakatifu anakuonyesha zambi katika maisha yako. Hivi utakuwa na maisha ya furaha na ushindi. 

UTEGEMEE ROHO MUTAKATIFU KUENDELEA KUKUONGOZA NA KUKUJAAZA. HIVI YESU KRISTO ATAKUWA BWANA NA MUTAWALA WA KITI CHA MAISHA YAKO WAKATI WOTE.


UAMINI MUNGU NA AHADIZAKE KATIKA BIBLIA 

Mukristo anaishi maisha yanayojaa na Roho Mutakatifu kwa imani tu. 

Wakati Roho Mutakatifu anaongoza maisha yako, utakuwa hivi: 
1. Matunda ya Roho Mutakatifu yatazidi kuonekana katika maisha yako. 
Wagalatia 5:22-23 
2. Maombi yako yatasikiwa na Mungu kila siku. Yakobo 5:16. 
3. Utaenaelea kufahamu Biblia. 2 Timoteo 3:16 
4. Utakuwa na uwezo wa Mungu, kumushuhudia. Matendo 1:8 
5. Utakuwa na uwezo wa Mungu, kushinda majaribu na zambi. 1 Wakorinto 10:13
6. Utaendelea kuishi maisha ya Mukristo anayejazwa na Roho Mutakatifu kwa imani. Waebrania 11:6, 1 Yoane 5:1-5 
7. Utategemea Mungu na ahadi zake. 2 Petro 1:3-11 
8. Utashinda pepo wachafu na Shetani. 1 Yoane 4:1-4

Sasa jambo linalokuha ni hili:


INAFAA KWENDA KANISANI 
Kuni zinawaka vizuri zikiwa pamoja. Ukitosha kuni moja na kuweka pembeni, itaanza kuzimika. Vivyo hivyo, itakuwa nguvu kuwa na maisha ya kiKristo pekee yako. 

Ni sharti kujiunge kwa watu wanaokubali Yesu Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wao. 

Uhuzurie kanisa, kwenye watu wanaoamini UKWELI wa Biblia na kutii Bwana Yesu. Waebrania 10:25.


KAMA KITABU HIKI KIMEKUSAIDIA, UKILETE KWA MUTU MWENGINE A 0 UMUSOMEE

LIFE  BUTEMBO, B.P. 5, ZAIRE 

Kimeanclikwa na Dr. Wm. Bright 
 Haki ya kunakili The LIFE Ministry